Alhamisi hii ya tarehe 13 Agosti 2026, shirika la FOMI limepokea wageni kutokea Burkina Faso wakiongozwa na Mheshimiwa waziri wao mambo ya nje Karamoko Jean Marie Traoré. Kwenye neno lake la ukaribisho, makamu Mkurugenzi mkuu wa FOMI alijulisha kwamba FOMI ni mmoja wapo wa matawi yanayo unda shirika la Itracom Holding na kutambua uwepo wa makamu mkurugenzi mkuu wa Itracom Holding bwana Nyandwi Jean Joseph ambae amechukua na fasi na kueleza shughuli za shirika la Itracom Holding na kutaja kwamba miongoni mwake kuna FOMI ambayo inatengeneza mchanganyiko wa mbolea asilia na madini,mbolea zenye sifa ya kipekee kwa kuzalisha sana na kurudisha rutuba ya ardhi tofauti na mbolea za zamani ambazo zimekua zikiathiri ardhi.

Makamu Mkurugenzi mkuu wa FOMI, Ir Herménégilde Manyange nae aliwaeleza wageni historia ya FOMI, mafanikio yake toka lianzishwe mwaka wa 2019.

Waziri wa Burkina Faso wa mambo ya nje nae alieleza kua ziara yao ni katika makubaliano ya kuweka kamati shirikisho ya nchi mbili jambo lililoagizwa na maraisi wawili(Burkina Faso na Burundi). Kwa mjibu wake, waziri Jean Marie, Burundi kuna fursa ambazo zinaweza kuchangia kujenga uchumi wa afrika.
Alieleza kuwa Burkina Faso wana masilahi kwa mbolea kwani raia wake wengi ni wakulima. Kwa ufupi alifurahishwa na kuona kwamba Afrika wana mahitaji yanayofanana na uwezo wakukidhi mahitaji hayo wakijitegemea kama waafrika jambo ambalo linaenda sambamba na maono ya raisi wa Burkina Faso Kapiteni Ibrahim Traoré.
