Kwenye warsha ilioabdaliwa na MAC leo alhamisi kwenye Hoteli ya source du Nil jijini Bujumbura ili watasmini shughuli ambazo wamezifanya toka mwaka wa 2022 hadi 2025,walioshika na fasi kuchangia wote wameshukuru mafundisho waliopewa na wafanyakazi wa FOMI kuhusu namna ya kurutubisha ardhi kwa kutumia mbolea za FOMI.
Mwenyekiti #MAC NDUWIMANA Aimé Pascal alijurisha kwamba katika miaka hiyo ndipo walikaribia viongozi wa FOMI ili wasaidie wanachama wa MAC kwa kuwapatia mafunzo yanyohusu kufanya kilimo cha kisasa wakitumia mbolea za FOMI.Alitoa mifano ya ziara zilizofanyika kwenye mikoa mbalimbali ambapo wafanyakazi wa FOMI walikua wakikuta wakulima kwenye shughuli mashambani mwao na kuwafundisha.Toka viongozi wa madhebu wanachama wa MAC wameanza kutekeleza kile walichofundishwa na wafanyakazi wa FOMI,uzalishaji kwenye segita ya kilimo uliongezeka kwenye mashamba yao.Waliochukua na fasi wakachangia katika viongozi wa dini,wameshukuru kuona kwamba mbolea ya FOMI ilisababisha ongezeko la uzalishaji,kupunguza tindikali ardhini kwa kutumia chokaa ya kilimo ambayo inatengenezwa na kiwanda cha FOMI.
Katika badhi ya maswali walioyauliza,waliomba kupata mbolea kwa wakati kwa sababu inapokawia inapelekea uzalishaji kupungua.Makamu Mkurugenzi mkuu wa FOMI Ir Herménégilde MANYANGE alijurisha kwamba FOMI na MAC wataendelea kushilikiana ili shughuli ziendelee kupiga hatua mbele.Kwa upande wa wizara ya kilimo,ufugaji na mazingira,naibu waziri ambae alimuwakilsha waziri kwenye warsha hio bwana Butoyi Leonard alifahamisha kuwa ucheleweshaji wa mbolea hutokea kwenye idadi kubwa ambayo huongezeka mwaka baada ya mwingine ya wanayoyihitaji.Amewatia moyo akisema kuwa FOMI imesha jenga kiwanda kingine ili waweze kutengeneza kiasi cha mbolea ambacho ni kikubwa ukilinganisha na mahitaji ya wakulima na pia kuweza kupa ya kuuza inje