dustra
  • Nyumbani
  • Kuhusu Sisi
  • Bidhaa Zetu
    • FOMI-IMBURA
    • FOMI-TOTAHAZA
    • FOMI-BAGARA
    • CHAUX AGRICOLE
  • Timu
  • Habari
  • Wasiliana Nasi
  • Lugha
    • ENG
    • FRA
    • KIR

Kiongozi wa taasisi inayosimamia mbolea nchini Tanzania anasifu jinsi kiwanda cha FOMI kinavyozalisha na kusambaza mbolea kuwafikia wakulima. - FOMI-Sw

  • Home
  • Kiongozi wa taasisi inayosimamia mbolea nchini Tanzania anasifu jinsi kiwanda cha FOMI kinavyozalisha na kusambaza mbolea kuwafikia wakulima.
  • Disemba 2, 2025
  • FOMI

Jumatatu, tarehe 8 Julai 2025, kampuni inayozalisha mbolea ya kikaboni na ya madini, FOMI, ilipokea wageni kutoka nchini Tanzania. Walikuwa wakiongozwa na mkuu wa taasisi ya udhibiti wa mbolea nchini Tanzania, Tanzania Fertilizer Regulatory Authority, Dkt. Antony Diallo.

Katika hotuba yake ya ukaribisho, Mkurugenzi Mkuu wa FOMI, Simon Ntirampeba, aliwapatia ufupisho wa historia ya kiwanda.
Mkurugenzi Mkuu alieleza jinsi wanavyofanya kazi pamoja na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Mazingira katika kuwasaidia wakulima kupata mbolea.
Alisema kuwa Serikali ndiyo inawaalika wakulima kujiandikisha, na baadaye kulipia kiasi cha mbolea kulingana na kiwango na aina wanayoihitaji.
Alieleza pia kuwa malori ya FOMI ndiyo husambaza mbolea hadi katika maeneo mbalimbali nchini ili wakulima wapate mbolea karibu na maeneo yao.

Baadhi ya wageni walitoa maswali, wakitaka kujua ikiwa mbolea inayozalishwa na FOMI inatosha kuwahudumia wakulima wote, na kama kuna viwanda vingine vinavyozalisha mbolea mbali na FOMI.
Mkurugenzi Mkuu alijibu maswali hayo mbalimbali.

Dkt. Antony Diallo, aliyekuwa akiongoza ujumbe huo, alisema kuwa walikuja kupata ujuzi ili waweze kujifunza mbinu za kushirikiana na kiwanda cha ITRACOM Fertilizer katika kuhakikisha mbolea inawafikia wakulima kwa urahisi.

Alieleza kuwa wamejifunza mambo mengi ambayo yatawasaidia katika kazi ya kusambaza mbolea kwa wananchi.
Aliwapongeza viongozi wa FOMI kwa jinsi wanavyoshirikiana na wizara pamoja na benki katika juhudi za kuwasogezea mbolea wananchi.

Mawaziri watatu (3) wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (RDC) walitembelea kampuni ya FOMI.

Leave a comment

Cancel reply

Recent Posts

  • Mkutano na waandishi wa habari wa kampuni ya Fomi kuhusu uzalishaji na usambazaji wa mbolea tarehe 31/12/2025.
  • MBOLEA YA FOMI IMEDHIRISHA KUWA NA UWEZO WA KURUDISHA RUTUBA ARDHI KWENYE SEHEMU NYINGI
  • Wizara ya kilimo,ufugaji na mazingira inatia moyo wakulima kuhusu ukosefu wa mbolea#FOMI
  • Timu ya Burundi Black Eagle ilikabiliana na ASAS Djibouti Télécom kutoka Djibouti.
  • Mawaziri watatu (3) wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (RDC) walitembelea kampuni ya FOMI.

Recent Comments

Hamna maoni ya kuonyesha.

Category

  • Uncategorized (6)

Wasiliana Nasi

  • Route de l'Aéroport(RN5)-Zone Mutimbuzi
  • info@fomi.bi

Bidhaa Zetu

  • FOMI-IMBURA
  • FOMI-TOTAHAZA
  • FOMI-BAGARA
  • CHAUX AGRICOLE

Saa za ufunguzi

  • Jumatatu :
    8.00 - 17.00
  • Jumanne :
    8.00- 17.00
  • Jumatano :
    8.00 - 17.00
  • Alhamisi - Ijumaa :
    8.00 - 17.00
  • Jumamosi :
    8.00 - 13.00
  • Jumapili :
    Imefungwa

© 2025 FOMI- Designed by Manix MUGISHA.

dustra